Jan 13, 2014

ARE YOU BORED OF HEAVYNESS?? CLICK HEREE FOR: TEN EASY WAYS TO LOSE WEIGHT


 
You know the drill when it comes to losing weight -- take in fewer calories, burn more calories. But you also know that most diets and quick weight-loss plans have about as much substance as a politician's campaign pledges. Here are more than 50 easy ways for you to finally lose the weight.
If you’re trying to drop a few pounds, don’t start off by trying to overhaul all your eating and exercise habits. You’re better off finding several simple things you can do on a daily basis—along with following the cardinal rules of eating more vegetables and less fat and getting more physical activity. Together, they should send the scale numbers in the right direction: down.
1. Indulge in fat releasing foods. They should help keep you from feeling deprived and binging on higher-calorie foods. For instance:
  • Honey. Just 64 fat releasing calories in one tablespoon. Drizzle on fresh fruit.
  • Eggs. Just 70 calories in one hard-boiled egg, loaded with fat releasing protein. Sprinkle with chives for an even more elegant treat.
  • Part-skim ricotta cheese. Just 39 calories in one ounce of this food, packed with fat releasing calcium. Dollop over a bowl of fresh fruit for dessert.
  • Dark chocolate. About 168 calories in a one-ounce square, but it’s packed with fat releasing fiber.
  • Shrimp. Just 60 calories in 12 large.
  • MORE: 13 fat releasing foods »
2. Treat high-calorie foods as jewels in the crown. Make a spoonful of ice cream the jewel and a bowl of fruit the crown. Cut down on the chips by pairing each bite with lots of chunky, filling fresh salsa, suggests Jeff Novick, director of nutrition at the Pritikin Longevity Center & Spa in Florida. Balance a little cheese with a lot of salad.
3. After breakfast, make water your primary drink. At breakfast, go ahead and drink orange juice. But throughout the rest of the day, focus on water instead of juice or soda. The average American consumes an extra 245 calories a day from soft drinks. That’s nearly 90,000 calories a year — or 25 pounds! And research shows that despite the calories, sugary drinks don’t trigger a sense of fullness the way that food does.
4. Carry a palm-size notebook everywhere you go for one week. Write down every single morsel that enters your lips—even water. Studies have found that people who maintain food diaries wind up eating about 15 percent less food than those who don’t.
Plus: Lose weight, ease digestion on our 21-Day Tummy diet »
5. Buy a pedometer, clip it to your belt, and aim for an extra 1,000 steps a day. On average, sedentary people take only 2,000 to 3,000 steps a day. Adding 2,000 steps will help you maintain your current weight and stop gaining weight; adding more than that will help you lose weight.
6. Add 10 percent to the amount of daily calories you think you’re eating, then adjust your eating habits accordingly. If you think you’re consuming 1,700 calories a day and don’t understand why you’re not losing weight, add another 170 calories to your guesstimate. Chances are, the new number is more accurate.
7. Eat five or six small meals or snacks a day instead of three large meals. A 1999 South African study found that when men ate parts of their morning meal at intervals over five hours, they consumed almost 30 percent fewer calories at lunch than when they ate a single breakfast. Other studies show that even if you eat the same number of calories distributed this way, your body releases less insulin, which keeps blood sugar steady and helps control hunger.
8. Walk for 45 minutes a day. The reason we’re suggesting 45 minutes instead of the typical 30 is that a Duke University study found that while 30 minutes of daily walking is enough to prevent weight gain in most relatively sedentary people, exercise beyond 30 minutes results in weight and fat loss. Burning an additional 300 calories a day with three miles of brisk walking (45 minutes should do it) could help you lose 30 pounds in a year without even changing how much you’re eating.
9. Find an online weight-loss buddy. A University of Vermont study found that online weight-loss buddies help you keep the weight off. The researchers followed volunteers for 18 months. Those assigned to an Internet-based weight maintenance program sustained their weight loss better than those who met face-to-face in a support group.
10. Bring the color blue into your life more often. There’s a good reason you won’t see many fast-food restaurants decorated in blue: Believe it or not, the color blue functions as an appetite suppressant. So serve up dinner on blue plates, dress in blue while you eat, and cover your table with a blue tablecloth. Conversely, avoid red, yellow, and orange in your dining areas. Studies find they encourage eating.

MOTHER AND 2 CHILDREN FOUND DIED



Police say they are not looking for anyone else in connection with deaths of woman, 33, and two young boys in Brent

A woman and two children aged five and seven months have died in an apparent murder-suicide.
The 33-year-old woman and two boys were found at 5.20pm on Thursday at their house in Brent, north-west London, and pronounced dead at the scene.
Police said officers were called by the London ambulance service to the address in Woodgrange Close, to reports of a woman and two children with injuries. When they arrived, the three were pronounced dead by medical staff.
Detectives are treating the children's deaths as murder and believe that the woman's death is not suspicious. They are not looking for anyone else in connection with the killings.
A spokesman for Brent council said: "The family were known to the council but it would be inappropriate to comment further while the police investigation is at such an early stage."
Neighbours expressed their shock at what had happened and said arguing was often heard coming from the flat.
Tashma Brown, 34, who lives next door, said the couple who lived at the address were Sakthivel Vageswaran and his wife Jeyavani Vageswaran.
She said: "She was a person you didn't see often. There was always shouting and arguing, three or four times in a month sometimes. Most of the time when they argued he would come outside to cool down."
Leslie Gotts, who has lived in Woodgrange Close for 18 years, said the family, who are believed to be of Sri Lankan origin, had lived in the first-floor flat in the house for about a year.
A neighbour had told him that the children's father had found their bodies along with his wife's, he said.
Gotts, 70, said: "I just couldn't believe what I was hearing. You freeze. It's a quiet road, a very mixed community. I think I only saw her once. She didn't look very unhappy to me."
A postmortem examination gave the woman's cause of death as compression of the neck, a Scotland Yard spokesman said last night. Postmortem examinations are expected to be carried out on the two children on Tuesday, he added.
Councillor Reg Colwill, who represents Kenton ward where the family lived, said: "I think everybody is the same – they are shocked at what has happened.
"If it's accurate that the woman took her own life she must have been at her wits' end and didn't ask for help, or didn't get the help she asked for. It's two young children. It's very sad."
Brown said she last heard the couple arguing the week before Christmas and also heard the woman getting upset on Tuesday or Wednesday about the baby crying in the house.
"She was shouting but it was in her own language. She sounded upset," Brown said.
She added that she rarely saw the family outside.
"As a mum with a child, I would only see her when she came out with her kids. I would never see her with the kids in the park walking around."
Brown added that she wanted to move following the discovery of the bodies.

READ: A STORY OF LONELY MOM


A mother has not slept for three days and nights watching over her sick child. When she closes her eyes for just a moment, Death comes and takes her child. The mother rushes into the street and asks a woman, who is Night, which way Death went.
"Death walks faster than the wind and never returns what he has taken."
"Tell me which way he went and I will find him!"
Night tells her to go into the forest, but first the mother must sing every lullaby that she has ever sung for her child. In the forest, a thorn bush tells her which way to continue, but only after she has warmed the bush by pressing it to her chest, causing her to bleed. The mother then reaches a lake that carries her across in exchange for her eyes, which she cries out.
The now blind mother reaches the greenhouse where Death cares for the flowers and trees, each one a human life. Here the mother finds the little sick plant that is her child, recognizing it by the sound of its heartbeat. The old woman who helps care for the greenhouse tells her, in exchange for her hair, that when Death comes, she must threaten to rip up the other flowers. Death will then be afraid for he must answer to God; only God decides when the plants are pulled up and planted in the garden of Paradise, where we do not know what happens.
Death comes carrying the child and when he asks the mother how she could have gotten there before him, she answers, "I am a mother." She threatens to rip out two of the flowers, but when Death asks her if she would make two other mothers as unhappy as she is, she immediately lets go.
Death gives her back her eyes and asks her to look into a well. Here she sees the futures of two children, one full of happiness and love, the other full of misery and despair. He says that one of these futures would be the future of her child, were it to live.
Then the mother screams in fear, "Which is my child! Rather carry my child into God's kingdom than allow it to suffer such a life."
Death says, "I do not understand. Do you want your child back or should I carry it away into the unknown?"
And the mother wrings her hands, gets down on her knees, and prays to God:
"Do not listen to me when I ask against your will! Do not listen to me, do not listen to me, do not listen to me!"
And Death leaves, carrying her child into the unknown land.

LULU MICHAEL AM “SURPRISE” MAMA KANUMBA


 

Stori: Hamida Hassan na Imelda Mtema
MSANII wa filamu, Elizabeth Michael ‘Lulu’, mwanzoni mwa wiki hii alimshangaza (surprise) mama wa mpenzi wake wa zamani, marehemu Steven Kanumba, Flora Mtegoa wakati alipokuwa akisherehekea miaka 58 tokea alipozaliwa.


Keki aliyoleta Lulu kwa ajili ya mama Kanumba.
Kumshangaza huko kumekuja baada ya Lulu kufika nyumbani kwa mama Kanumba, Kimara Temboni jijini Dar akiwa na bonge la keki, jambo ambalo mama huyo hakulitarajia.…
Stori: Hamida Hassan na Imelda Mtema
MSANII wa filamu, Elizabeth Michael ‘Lulu’, mwanzoni mwa wiki hii alimshangaza (surprise) mama wa mpenzi wake wa zamani, marehemu Steven Kanumba, Flora Mtegoa wakati alipokuwa akisherehekea miaka 58 tokea alipozaliwa.


Keki aliyoleta Lulu kwa ajili ya mama Kanumba.
Kumshangaza huko kumekuja baada ya Lulu kufika nyumbani kwa mama Kanumba, Kimara Temboni jijini Dar akiwa na bonge la keki, jambo ambalo mama huyo hakulitarajia.

Lulu akimpatia keki mama Kanumba.
“Yaani mama Kanumba alikuwa hajui kuwa Lulu anajua siku yake ya kuzaliwa, Lulu akatumia nafasi hiyo kumfanyia ‘sapraizi’,” alisema rafiki wa karibu wa Lulu aliyeomba hifadhi ya jina lake.

...Lulu akimlisha keki mama Kanumba.
Waandishi wetu waliokuwa eneo la tukio walimshuhudia mama Kanumba akiwa amepigwa na butwaa huku akilengwalengwa na machozi ya furaha. Mahojiano yalifanyika kama ifuatavyo;
Ijumaa: Hongera mama, sasa unatimiza miaka mingapi?
Mama Kanumba: Nimetimiza miaka 58.

Mama Kanumba akimlisha keki mama mzazi wa Lulu, Lucresia Karugila.
Ijumaa: Umejisikiaje kwa zawadi ya keki uliyoletewa na Lulu?
Mama Kanumba: Nimejisikia furaha sana kwa kweli, Lulu ni mwanangu, nimefarijika, kwa sababu watoto wangu hawapo, leo ningekuwa peke yangu lakini kama unavyoona, mama na mwanaye wamekuja toka asubuhi tunasherehekea nao kwa kula na kunywa na Lulu amegharamia kila kitu.
Baada ya swali hilo Ijumaa lilihamia kwa Lulu.

 
Kutoka kushoto: Flora Mtegoa, Lulu na Lucresia Karugila katika pozi.
Ijumaa: Ulijuaje leo ni siku ya kuzaliwa ya mama Kanumba?
Lulu: Nilijua katika maongezi siku sita zilizopita, kwani ilikuwa ni tarehe moja ya mwezi huu ambapo amezaliwa mama yangu mzazi na dada yangu.
Ijumaa: Kwa nini uliamua kumfanyia Sapraizi ya keki mama Kanumba?


Mama Kanumba akikata keki.
Lulu: Niliamua kumfurahisha kwa sababu ni siku yake ya kuzaliwa na sikufanya kwa sababu mwanaye hayupo, hata angekuwepo ningemfanyia tu.
Ijumaa: Asanteni, mama na Lulu tunawatakia maisha mema.


Flora Mtegoa akipozi na Lulu.

Dec 1, 2012

Rufaa kusikilizwa na majaji Salum Massati, Katherine Oriyo na Nathalia Kimaro.

RUFAA ya kupinga hukumu ya Mahakama Kuu ya Tanzania Kanda ya Dar es Salaam iliyompa ushindi Mbunge wa Ubungo, John Mnyika katika kesi ya uchaguzi dhidi yake, sasa imeiva.
Tayari rufaa hiyo imeshapangiwa jopo la majaji watu wa Mahakama ya Rufani watakaoisikiliza na kuitolea uamuzi na imepangwa kusikilizwa wiki ijayo.
Kwa mujibu wa ratiba ya vikao vya Mahakama ya Rufani, rufaa hiyo imepangwa kusikilizwa Desemba 7 mwaka huu.
Ratiba hiyo inaonyesha kuwa rufaa hiyo itasikilizwa na majaji Salum Massati, Katherine Oriyo na Nathalia Kimaro.
Rufaa hiyo ilifunguliwa Oktoba 25 mwaka huu na aliyekuwa mgombea wa ubunge katika Jimbo la Ubungo kupitia tiketi ya Chama Cha Mapinduzi (CCM), Hawa Ng’humbi, aliyekuwa mlalamikaji katika kesi ya msingi.
Mahakama Kuu katika hukumu yake iliyotolewa na Jaji Upendo Msuya Mei 24, 2012, ilitupilia mbali madai ya Ng’humbi ikisema alishindwa kuyathibitisha na badala yake, ikamthibitisha rasmi Mnyika kuwa mbunge halali wa jimbo hilo. Hata hivyo, Ng’humbi hakukubaliana na hukumu hiyo, ndipo akakata rufaa akiiomba hukumu hiyo itenguliwe.
Ng’humbi anayewakilishwa na Wakili Issa Maige, katika rufaa yake hiyo ameorodhesha hoja 10 za kupinga hukumu hiyo, akidokeza kile anachokiona kuwa ni udhaifu katika hukumu hiyo.
Pamoja na mambo mengine, Ng’humbi anadai kuwa Jaji aliyesikiliza kesi ya msingi na kutoa hukumu hiyo, alikosea katika kutafsiri sheria na kupima ushahidi wa pande zote.
Ng’humbi anadai kuwa jaji alikosea kisheria na kiukweli kwa kusema kuwa makosa yaliyobainika katika ujumlishaji na kuhesabu kura na kusababisha kuwapo kwa kura 14,854, zisizohesabiwa hayakuathiri matokeo ya uchaguzi.
Anadai kuwa aliweza kuthibitsha kuwapo kwa makosa katika mchakato wa uchaguzi yaliyosababisha kuwapo kwa kura 14, 854 zisizohesabiwa na kwamba jaji alikosea kisheria na kiukweli kwa kutokuhamishia kwa mdaiwa, jukumu la kuelezea sababu za kuwapo kwa dosari hizo.
“Jaji alikosea kisheria na kiukweli kusema kwamba kura 14,854, ambazo hazikuhesabiwa zilitokana na makosa ya kibinadamu, bila kuwepo na ushahidi kuhusu hilo katika kumbukumbu za mahakama.”
Katika hoja nyingine, Ng’humbi anadai kuwa jaji alikosea kisheria na kiukweli kwa kusema kuwa hazikutumika kompyuta ambazo hazikuwa zimeidhinishwa na mamlaka husika katika kujumlisha na kura.

Jaji Mkuu: Siku ya kesi ya Lema nitakuwa nje ya nchi, sijajitoa



JAJI Mkuu, Mohamed Chande Othman ameeleza sababu za kutokuwa kwenye jopo la majaji waliopangwa kusikiliza kesi ya aliyekuwa mbunge wa Chadema mkoani Arusha, Godbless Lema.
Jaji mkuu, alitoa maelezo haya jana alipozungumza na gazeti hili katika mahojiano maalumu kwenye mahafali ya 12 ya Chuo cha Uongozi wa Mahakama Lushoto (IJA).
“Ngoja nitolee ufafanuzi suala hilo ili jamii itambue utaratibu wa uendeshaji wa Mahakama ya Rufani, ambayo ina majaji 16 nchini,” alisema Jaji Othman.
Jaji Othman alisema kimsingi hajajitoa kushughulikia kesi hiyo, ila siku ambayo kesi hiyo inatajwa, atakuwa nchini India kuhudhuria Mkutano Mkuu wa 13 wa Majaji Wakuu Duniani.
Maelezo hayo ya Jaji Chande yamekuja siku tatu baada ya gazeti hili kuripoti kuwa, mkuu huyo wa mhimili wa Mahakama nchini amejitoa kusikiliza kesi hiyo na nafasi yake imechukuliwa na Jaji Bernard Luanda.
“Kwanza ifahamike kwamba, jaji wa Mahakama ya rufani hana ubia na kesi yoyote kwa mujibu wa utaratibu. Jaji yeyote kati ya majaji 16 wa mahakama ya rufani nchini ana mamlaka ya kusikiliza kesi yoyote ya rufani,” alieleza Jaji Othman.
Jaji Othman alifafanua kuwa, rufani ya Lema ni miongoni mwa kesi tatu za uchaguzi zilizobaki ambazo kwa mujibu wa taratibu za kisheria, huanza kusikilizwa baada ya muda wa mwaka mmoja na hukumu yake ni lazima itolewe ndani ya mwaka mmoja tangu kuanza kwake.
“Hivyo basi, kwa vile Jaji yeyote wa Mahakama ya Rufaa anaweza kuisikiliza kesi hiyo, hakukuwa na sababu inisubiri mimi,” alisema.
Jaji Othman alitaja kesi nyingine za uchaguzi zitakazoanza kufanyiwa vikao vya rufani na jopo la majaji wa Mahakama ya Rufani kuwa, ni ile ya Jimbo la Ubungo kati ya Hawa Ng’umbi na John Mnyika ambayo itakuwa chini ya jopo la majaji watatu; Jaji Nathalia Kimaro, Jaji Salum, Salum Masati na Jaji Katherine Oriyo.
Nyingine ni ya Jimbo la Ilemela ya Yusuph Yussuph Masengela Lupilya na wenzake wawili dhidi ya Highness Kiwia na wenzake wawili, ambayo itakuwa chini ya jopo la Majaji Januari Msofe, Jaji Beard Luanda na Jaji Salum Massati.
Alisema rufani ya Lema haijaanza kusikilizwa kwa jaji yeyote, hivyo yeye asingeweza kujitoa kwa kuwa hajapangiwa.
“Kinachotatiza hapa ni kwamba, watu wanaifungamanisha rufani hii na ile ya Arusha ambayo mimi nilikuwa miongoni mwa jopo la majaji kama mwenyekiti.

UZINDUZI WA ALBAM YA MASHUJAA NA JB MPIANA YAINGIA DOSARI.....MMILIKI AZIMIA NA KUKIMBIZWA HOSIPITALI


Watu  mbalimbali wakiwa wamelizunguka jenereta leo usiku
  Mwanamuziki kutoka DRC-Congo,JB Mpiana akitumbuiza jukwaani mara baada ya kupanda mnamo majira ya saa tisa kasoro,baada ya hitilafu za umeme kwenye jenerata kurekebishwa.
-------------------------
SHOO YA UZINDUZI WA ALBAM YA PILI YA MASHUJAA BAND, ILIINGIA DOSARI NA KUTAKA KUSHINDWA KUFANYIKA  KATIKA VIWANJA VYA LEADERS CLUB USIKU HUU KUTOKANA NA KATIZO LA UMEME LA MARA KWA MARA LINALOSABABISHWA NA JENERETA LINALOTUMIWA KUTOA UMEME KATIKA VIWANJA VYA LEADERS CLUB,JIJINI DAR.

HALI HIYO ILIPELEKEA MMILIKI WA BENDI YA MASHUJAA,MAMA SAKINA KUPOTEZA FAHAMU NA KUKIMBIZWA HOSPITALI.

UBUNGE NI KAZI YA KIBWEGE..." AFANDE SELE KATIKA XXL JANA

Ubunge ni kazi ya 'kibwege' watu wamekuchagua ili uwatumikia kwa hiyo unatakiwa kuwa mtumwa wa watu wako kwa kuwa karibu na kufanya kile wanachokihitajiwao na siyo kukalia kiti hicho kwa niaba yako na ndugu zako, inanishangaza sana mtu anachaguliwa ndani ya miaka miwili tayari anamiliki Vogue sasa huu ka siyo wizi ni nini" Afande Sele

Nov 29, 2012



POLISI AFUKUZWA KAZI BAADA YA KUMBAKA MTUHUMIWA WA KIKE


JESHI la Polisi mkoani Mbeya limemfukuza kazi askari wake Enock Daffa (22) kwa tuhuma za kufanya  mapenzi na mtuhumiwa wa kike mwenye umri wa miaka 25 katika Kituo cha Polisi cha Mji mdogo wa Tunduma, Wilaya ya Momba, mkoani hapa. 

Kwa mujibu wa Kamanda wa Polisi Mkoa wa Mbeya, Athuman Diwani, askari huyo alitenda kosa hilo Novemba 21,2012 na kwamba mtuhumiwa aliyefanya naye mapenzi alikuwa akikabiliwa na kosa la wizi.
 
Kamanda Athumani alisema kuwa mbali ya kufukuzwa kazi askari huyo tayari amefikishwa katika Mahakama ya Wilaya ya Mbozi ili sheria iweze kuchukua mkondo wake.

Aidha alisema kuwa hali kama hiyo haitaweza kuvumiliwa na Jeshi la Polisi na kwamba atakayebainika kufanya tukio kama hilo adhabu yake itakuwa ni kufukuzwa kazi.
 
Kamanda huyo alitoa wito kwa askari polisi kufanya kazi kwa kufuata sheria na kanuni za Jeshi la Polisi kama mwongozo unavyowaagiza ili kulinda maadili ya Jeshi la Polisi ambacho ndicho chombo kinachotumika na wananchi katika kuzisimamia sheria.
 
Akizungumzia tukio hilo, baba mzazi wa askari huyo alisema kuwa kitendo alichofaya mtoto wake si cha kiungwana ambacho pia kimetia fedheha familia yake pia kwa jeshi la Polisi ambalo limepewa dhamana ya kutunza usalama wa raia na mali zake.

MIKOPO KWA WANAFUNZI AMBAO NI WATOTO WA VIGOGO YAPIGWA MARUFUKU


BODI ya Mikopo ya Elimu ya Juu Zanzibar, imeagizwa kuacha mara moja upendeleo wa kutoa mikopo kwa watoto wa vigogo kwani kufanya hivyo ni kwenda kinyume na malengo ya kuanzishwa kwa taasisi hiyo.

Makamu wa Kwanza wa Rais Zanzibar, Seif Sharif Hamad alitoa agizo hilo jana alipozungumza na uongozi na watendaji wa Bodi ya Mikopo ya Elimu ya Juu Zanzibar Mnazi Mmoja mjini hapa.

Seif alisema yapo malalamiko mengi kutoka kwa wananchi na wazazi, kwamba Bodi hiyo inatoa mikopo kwa watu ambao hawana sifa, wakiwamo watoto wa vigogo.

“Yapo malalamiko mengi ya wananchi na wazazi kuhusu Bodi hii, ikiwamo kutoa mikopo kwa njia ya upendeleo kwa watu ambao hawana sifa na watoto wa wakubwa,” alisema.

Alikumbusha watendaji wa Bodi hiyo, kwamba taasisi hiyo imeanzishwa kusaidia maendeleo ya watoto masikini wasiokuwa na uwezo wa kumudu gharama za masomo.

“Hayo ndiyo malengo ya kuanzishwa kwa Bodi ya Mikopo ya Elimu ya Juu, kutoa mikopo kwa watoto wa masikini wasiokuwa na uwezo wa kugharimia masomo,” alisisitiza.

Alisema wakifanikiwa kutekeleza malengo hayo kwa kiasi kikubwa, Bodi itatoa mikopo kwa wanafunzi wengi na kuepusha urasimu na kutiwa shinikizo kutoka kwa wakubwa.

Awali Mkurugenzi Mtendaji wa Bodi hiyo, Iddi Khamis alisema Bodi imezidiwa na maombi na mahitaji ya wanafunzi wa elimu ya juu wanaohitaji mikopo hiyo wakiwamo wenye sifa.

Akifafanua, Iddi alisema kwa sasa vipo vyuo vya elimu ya juu vinne vikiwa na wanafunzi wenye mahitaji ya mikopo kwa ajili ya kujiendeleza zaidi, lakini Bodi haina uwezo huo.

“Tumezidiwa na idadi ya wanafunzi wanaohitaji mikopo ya elimu ya juu sasa…vipo vyuo vikuu vinne vyenye wanafunzi wanaohitaji mikopo,” alisema.

Hata hivyo, Khamis alisema kwa bajeti ya mwaka 2012/13, Bodi imeongezwa bajeti ya fedha kutoka Sh bilioni 4 hadi Sh bilioni 8 ingawa bado hazitoshi.

Alifafanua, kuwa maombi ya mikopo kwa wanafunzi yameongezeka kutoka 800 hadi 1,800 na Bodi imeshindwa kuwapa mikopo wanafunzi hao wa ziada hivi sasa.

Hata hivyo, wanafunzi wanaokosa mikopo kutoka Bodi hiyo bado wana nafasi ya kuomba kupitia Bodi ya Mikopo ya Elimu ya Juu ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania.

Nov 24, 2012

Chadema uongozi balaa

 



CHAMA cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema), kimeitafutia dawa migogoro inayotokana na baadhi ya makada wake kuonyesha nia ya kuwania urais na ubunge mwaka 2015, baada ya kuanzisha utaratibu maalumu wa wanachama wake kugombea nafasi mbalimbali za uongozi.

Kwa mujibu wa taarifa zilizolifikia gageti  hili, mpango huo unakuja wakati Naibu Katibu Mkuu wa chama hicho, Zitto Kabwe ametangaza nia ya kugombea urais katika uchaguzi mkuu ujao, kitendo ambacho kiliwashtua vigogo wa chama hicho akiwamo mwasisi wake, Edwin Mtei.

Mara kadhaa Mtei amekuwa akimwonya Zitto kuwa kitendo chake cha kutangaza nia yake ya kugombea urais kitasababisha mzozo na mpasuko ndani ya chama hicho.

Mtei amekuwa akisema kuwa Zitto anatakiwa kuwaunganisha wanaChadema na siyo kuwagawa, au kuwavuruga na kwamba siyo shida kuonyesha hisia za kuwania urais, lakini tatizo ni kuwa hali hiyo inatengeneza mzozo mkubwa.

Mtei ambaye aliwahi kuwa Waziri wa Fedha na Gavana wa Benki Kuu (BOT) enzi za utawala wa Mwalimu Julius Nyerere, alisema wakati mwafaka ukiwadia, Chadema kitaamua ni nani mwenye sifa za kugombea urais akisema kina utaratibu wake wa kuwapata wagombea mbalimbali wa uongozi.

Akizungumza wakati akijibu hoja mbalimbali katika mtandao wa Jamii Forum katikati ya wiki hii, Zitto ambaye pia ni Mbunge wa Kigoma Kaskazini, alisema viongozi wa chama hicho walikutana mjini Morogoro hivi karibuni na kutengeneza utaratibu wa watu kutangaza nia wanapotaka kugombea nafasi yoyote ya uongozi.

“Nadhani huu ni uamuzi mzuri wa chama maana watu wengine wana wasiwasi usio na msingi wowote kwamba kuwa na wagombea wengi kwenye chama ni kuvuruga chama,” alisema Zitto na kuongeza:

“Lakini watu haohao wanashangilia kweli wakiona demokrasia inavyotekelezwa kwenye nchi nyingine kama Marekani.”

Alisema kuwa tatizo la Watanzania wanapenda kuona demokrasia inatekelezwa, lakini wao wanaogopa kuitekeleza, hivyo mwongozo kwa wagombea ambao walipitisha Morogoro utasaidia sana.

“Uamuzi wa Morogoro kuhusu mwongozo kwa wagombea utatusaidia sana kuondoa mashaka kama haya,” alisema Zitto.

Mwananchi Jumapili lilipomuuliza Mkurugenzi wa Habari na Uenezi wa chama hicho, John Mnyika kuhusu jambo hilo  alionyesha kutofahamu lolote kuhusu utaratibu huo, wala ulipofanyika huo mkutano wa Morogoro.

“Mkutano upi wa Morogoro?” alihoji Mnyika. Alipoelezwa kuwa suala hilo lilizungumzwa na Zitto katika Mtandao wa Jamii Forum alisema: “Muulize kwanza Zitto akupe ufafanuzi ni kikao gani cha chama, pia juu ya huo utaratibu, akikueleza ndiyo urudi tena kwangu.”

Juhudi za kumpata Zitto kueleza kwa undani kuhusu utaratibu huo hazikuzaa matunda, kwani simu yake ya mkononi ilikuwa ikiita bila majibu, baadaye kuzimwa kabisa.

Akizungumzia azma yake ya kuachana na ubunge kama alivyoahidi mwaka 2005 kuwa, atagombea vipindi viwili pekee Zitto, alisema kuwa aliwaambia wapigakura wake kwamba nia yake ni kuwa rais wa nchi.

“Nia yangu ni kupisha wengine nao wakimbize kijiti cha maendeleo ya jimbo letu na mkoa wetu,” alisema Zitto na kufafanua, “ Nimeshasema mara kwa mara kwamba ukiachana na siasa kazi ninayoipenda zaidi ni ualimu.”

Alisema kuwa akiachana na ubunge atakwenda kufundisha kwa kuwa anapenda kufanya tafiti, kusoma, kuandika na kufundisha.

“Hivi sasa tunaandaa mpango wa kuanzisha Chuo Kikuu cha Ziwa Tanganyika (Lake Tanganyika) mkoani Kigoma, nitafurahi kama nitakuwa mmoja wa wahadhiri wa mwanzo wa chuo hiki,” alisema Zitto.

Katika uchaguzi Mkuu wa mwaka 2005, Mwenyekiti wa Chama hicho, Freeman Mbowe alisimama kugombea nafasi ya urais akishindana na Rais Jakaya Kikwete ambaye alikuwa akisimama kwa mara ya kwanza.

Mwaka 2010, Katibu Mkuu wa chama hicho, Dk Willbrod Slaa aligombea nafasi hiyo na kuibuka mshindi wa pili kwa kupata asilimia 26.34 nyuma ya Rais Kikwete ambaye alipata asilimia 61.17.

Hivi sasa tayari kumetokea maneno ya chinichini miongoni mwa wabunge waliopo madarakani wakiwatuhumu baadhi ya wanachama wa chama hicho ambao wameaanza kuingia katika majimbo yao kutaka kugombea viti hivyo katika uchaguzi mkuu wa mwaka 2015.

Wabunge hao wanahoji kama wanachama hao wanaofanya hivyo wanataka kugombea ubunge katika uchaguzi ujao ili kukifanya chama kiongeze idadi ya wabunge bungeni, kwa nini wasiende kugombea katika majimbo ambayo hayana  wabunge wa chama hicho?

Vilevile, chama hicho kilipata msukosuko katika mchakato wa kupata wabunge wa Viti Maalumu katika uchaguzi uliopita na kulazimika kuweka vigezo ambavyo viliondoa manung’uniko hayo.

Baadhi ya vigezo hivyo ni elimu, mchango wa mgombea katika chama, wanawake waliogombea katika majimbo na uzoefu katika ubunge.

Nov 23, 2012

MAMBA AUA MWANAFUNZI NAKUJERUHI BABA MWANZA

 MWANAFUNZI mmoja Pascal Abudallah (14), wa Shule ya Msingi Nantare ameuawa na mamba kijijini hapo.

Afisa Mtendaji wa Kata ya Ngoma, Mwanza vijijini, Khamisi Ndaro amethibitisha kutokea kwa kifo hicho na akaongeza kwamba kilitokea saa 1.30 usiku mwishoni mwa wiki iliyopita na tayari mtoto amezikwa kijijini hapo.


Aliongeza kuwa licha ya kifo cha mtoto huyo, baba mmoja aitwaye Mtimba Manyeye (64) naye alipoteza kidole cha mkono wa kushoto baada ya kushambuliwa na mamba akiwa kando ya Ziwa Victoria.


Aidha, Afisa Mtendaji Ndaro alisema wanyamapori wamekuwa wakisumbua wananchi na akatoa mfano wa nyani ambao wapo zaidi ya 1,000 nao wamekuwa  wakisumbua sana wakulima wa eneo hilo kwani wameharibu zaidi ya hekari 150 za mashamba yao, hivyo kuwafanya kukata tamaa kuendelea kulima.


“Maofisa wa wanyamapori wamekuwa wakifanya msako lakini wanyama hao wanaendelea kuwa tishio kwa raia,” alisema Ndaro.

MIMI SI MTUMIAJI WA MADAWA YA KULEVYA".....LORD EYEZ

Habari mpya  kutoka kwa Lord Eyez baada ya kuchonga nasi  kuhusiana na watu kumuhusisha na utumiaji wa Madawa ya kulevya aliweza kufunguka na kuweka wazi kwa  kusema,“Kiukweli mimi sijihusishi kabisa na utumiaji wa madawa ya kulevya na wala si support watu watumie kwani utumiaji wa madawa ni hatari ”- Lord Eyez.

Nov 21, 2012

Sindano uzazi wa mpango balaa

UTAFITI umebaini kuwa sindano za uzazi wa mpango zinachangia kasi ya maambukizi ya virusi vya Ukimwi kwa kuwa zina vichocheo vingi ambavyo vinahuisha virusi vya Ukimwi katika nyumba ya uzazi na kuvipa nguvu ya kusambaa.

Inaelezwa kuwa walio katika hatari zaidi ya maambukizi hayo ni wanawake walioko katika ndoa kwa kuwa ndiyo wanaotumia zaidi sindano hizo.

Utafiti huo uliofanywa na wanasayansi wa Marekani na kuripotiwa na gazeti la The Guardian la Uingereza, umebaini kuwa wanawake wanaotumia sindano za uzazi wa mpango wapo katika hatari mara mbili ya kupata maambukizi ya Ukimwi au kuwaambukiza wenzi wao, kuliko wengine.

Katika utafiti huo uliofanywa katika nchi saba zinazoendelea barani Afrika ikiwamo Tanzania, wanasayansi hao kutoka Chuo Kikuu cha Washington, walipendekeza ushauri zaidi utolewe kwa wanandoa kabla mtu hajajiingiza kwenye matumizi ya sindano kama njia ya kupanga uzazi.

Utafiti huo ulifanyika kwa wanandoa 3,790 kutoka nchi za Tanzania, Afrika Kusini, Zimbabwe, Uganda, Kenya, Rwanda na Botswana, ulichapishwa kwa mara ya kwanza katika Jarida la Afya la Lancet kabla ya kunukuliwa na gazeti la The Guardian.

Utafiti umebaini pia kuwa zaidi ya wanawake 140 milioni duniani wanatumia njia mbalimbali za uzazi wa mpango, huku wanandoa wengi katika nchi za Kusini mwa Jangwa la Sahara, wanaoishi na VVU wakichagua kutumia sindano kama njia ya kuzuia mimba zisizotarajiwa.

Wanasayansi hao walikusanya taarifa kati ya wanandoa 3,790 ambao mmoja wao anaishi na VVU na mwenza wake akiwa hana maambukizo.

Aidha, wanawake ambao wanaishi na VVU na wanatumia sindano hizo pia walikuwa katika hatari zaidi ya kuwaambukiza wenzi wao.

Vipimo vilionyesha kuwa sindano hizo ambazo zina vichocheo ambavyo vinavipa nguvu virusi ndani ya nyumba ya uzazi (cervix).

Imeelezwa kuwa njia za uzazi wa mpango zinazohamasishwa zaidi na kupendwa zaidi na wanawake ni sindano, ambazo wanawake wanasema kuwa zinadumu kwa muda mrefu na zinaweza kutumika bila ya ruhusa au mume kufahamu.

Kiongozi mkuu wa utafiti huo, Renee Heffron wa Chuo Kikuu cha Washington alisema sindano za uzazi wa mpango zina vichocheo vingi ambavyo huvihuisha vijidudu vya Ukimwi katika nyumba ya uzazi na kuvipa nguvu ya kusambaa.

 “Ni vyema sasa kama tutasisitiza njia za uzazi wa mpango ambazo ni salama zaidi kama vile mipira ya kiume au njia nyingine ambazo hazina vichocheo (hormones) au zina kiasi kidogo cha vichocheo,” alisema Dk Heffron.

Mwanasayansi mwingine, Charles Morrison wa Kituo cha Afya cha Durham, nchini Marekani alisema uhamasishaji wa matumizi ya sindano za uzazi wa mpango unachochea maambukizi zaidi katika nchi za Jangwa la Sahara.

“Ushauri wangu kwa nchi zinazoendelea ni kuacha matumizi ya njia za uzazi wa mpango zenye vichocheo, ili tupunguze maambukizi, jibu la tatizo hili linatakiwa litafutwe sasa, nchi zinazohusika zinatakiwa zishiriki katika hili,” alisema.

Alivitaka vituo vya afya vitoe ushauri kwa wanawake kutumia kondomu badala ya sindano au vidonge.

Mara nyingi watu wanaotumia vidonge, wengi si wanandoa, mtu anayemeza vidonge vya kuzuia mimba anaogopa zaidi mimba, si Ukimwi.

Huchoche hamu ya mapenzi

Mfamasia katika Kitengo cha Dawa kwa watu wanaoishina VVU katika Hospitali ya Amana, Christopher Masika alisema anaafiki kuwa sindano na hata vidonge vinaweza kuwa ni sababu inayochochea maambukizi kwa sababu ya uhuru.

“Ninachokiona mimi katika hilo ni uhuru. Mtu anapotumia sindano huwa huru kufanya ngono kwa kuwa hana hofu ya mimba, hicho kinaweza kumfanya apate maambukizi kwa urahisi, tofauti na anapotumia kondomu,” alisema.

Alisema wapo baadhi ambao wakitumia sindano hizo vichocheo vinawafanya wapate hamu zaidi ya kufanya mapenzi, hivyo huanza kutembea na wanaume wengine.

Aliongeza kuwa mtu anayeishi na VVU akizuia mimba kwa njia ya sindano, ni rahisi kupata maambukizi mapya kutoka kwa mwenza wake.

Masika alisema wanawake wapewe elimu zaidi kwani wapo ambao wanadanganywa kuwa njia za uzazi wa mpango kama sindano, povu zinaweza kuzuia maambukizi, jambo ambalo si la kweli.

Wakati huohuo baadhi ya wanandoa wanaoishi na VVU wanaopata matibabu katika Hospitali ya Amana wamesema kuwa tangu waanze kutumia dawa za kupunguza makali ya Ukimwi (ARVs) hamu ya kufanya mapenzi imeongezeka kwa kasi kubwa.

Mkuu wa Kitengo cha Utafiti cha Tume ya Taifa ya Kudhibiti Ukimwi (Tacaids), Dk Arodia Mulokozi, alisema taasisi yake haiwezi kuzungumza lolote kuhusu utafiti huo, badala yake alilitaka Mwananchi kuzungumza na Kitengo cha Afya ya Uzazi wa Mpango cha Muhimbili.

“Hatuhusiki na masuala ya uzazi wa mpango, nafikiri unaweza kuzungumza na Kitengo cha ‘Reproductive Health’ cha Muhimbili,” alisema Dk Mulokozi.

Waziri wa Afya hakupatika, lakini msemaji wa wizara hiyo, Nsachris Mwamwaja alisema ni mapema mno kuchangia kuhusu utafiti huo, atafanya hivyo pindi atakapopata taarifa zaidi.

Mratibu wa Mpango wa  Uzazi wa Mpango Tanzania (Umati), Dk Morris Hiza amekiri kuufahamu utafiti huo, lakini akaeleza kuwa haujajitosheleza na bado una maswali mengi.

“Nilikuwapo wakati Heffron anawasilisha utafiti wake mjini Geneva, lakini nakumbuka mkutano ule wa WHO (Shirika la Afya Duniani) uliukataa,” alisema.

Alieleza kuwa Heffton alifanya utafiti huo kwa nyani na wanawake makahaba pekee.

Nov 9, 2012

MJUE STAA WETU WA LEO!!


Akiwa ni mwenye kipaji katika kucheza kun fu, karete na michezo mingi inayofanan na hiyo kwa pamoja inajulikana kama martial arts alijifunza akiwa na umri wa miaka nane.
Alizaliwa Beijing tarehe 26 April 1963, Jet li alianza mafunzo ya kiutamaduni kwa kuingia kwenye martial arts akiwa na umri wa miaka 8. Akiwa ana umri wa miaka 11 alishinda mashindano ya kitaifa katika mchezo wa karate na miaka 8 baadae aliingia rasmi kwenye tasnia ya filamu. Filamu yake ya kwanza ilikuwa “shaolin temple” 1982.
Alitengeneza filamu nyingine “Born to defend” ambayo ilionesha uhalisia wa maisha ya binadamu ya kawaida lakini haikufanya vizuri sokoni. Li akatoa Shaolin Temple ya pili kabla hajafanya nyingine the folk hero, wong Fei – Hung  akiwa muongozaji , “Once upon a time in china” mwaka 1991. Mwaka 1992 na nyingine mbili 1993 ikiwemo “the Legend of Fong sai – Yuk” na moja 1997.
Jet li alitengeneza filamu inayoendana na filamu aliyotengeneza Bruce Lee ya “Fist of Fury” na yeye kuiita filamu yake “fist of legend” mwaka 1994. Wamarekani walianza kumfahamu alipotoa filamu iliyomtambulisha kwao ya “Lethal Weapon 4” mwaka 1998
Toka kipindi hicho alianza kuingia mikataba na Hollywood na kutoa filamu kama “Romeo must Die (2000)” “kiss of the Dragon” (2001), “Hero” (2002) “war” (2007) na Forbidden Kingdom” mwaka 2008 akiwa na Jackie Chan. Li pia alicheza “Mummy” Jomb of the Dragon Emperor mwaka huohuo
Mwaka 2010 alicheza filamu nyingine kama “ying yang” “Expendables” ambayo ilienda na kutoa Expendables 2 mwaka 2012 akiwa na wasanii wakongwe katika tasnia ya filamu Marekani Sylvester (Rambo), Bruce Wills, Arnold, Van Damme, Dolph na wengine wengi.Alioa mara mbili, mwaka 1987  alioa Huang Qiuyan na kubahatika kupata watoto wawili wa kike Si na Taimi kabla ya kuachana mwaka 1990. Mwaka 1999 alioa mke mwingine ambaye ni mwigizaji maarufu sana Nina Li Chi, waliyezaa naye pia watoto wawili Jane (2000) na Jada (2002)
Jet li alipata maafa Desember 2004, alipokuwa anamwokoa mwanae Jane katika moja ya hotel zake anazomiliki ilipotokea kimbunga cha tsunami na kubomoa jingo hilo. Ilisadikika amefariki dunia lakini yupo hai na alipona yeye na mtoto wake inga yeye aliteguka mguu na kupata majeraha madogo madogo.