Nov 9, 2012

MJUE STAA WETU WA LEO!!


Akiwa ni mwenye kipaji katika kucheza kun fu, karete na michezo mingi inayofanan na hiyo kwa pamoja inajulikana kama martial arts alijifunza akiwa na umri wa miaka nane.
Alizaliwa Beijing tarehe 26 April 1963, Jet li alianza mafunzo ya kiutamaduni kwa kuingia kwenye martial arts akiwa na umri wa miaka 8. Akiwa ana umri wa miaka 11 alishinda mashindano ya kitaifa katika mchezo wa karate na miaka 8 baadae aliingia rasmi kwenye tasnia ya filamu. Filamu yake ya kwanza ilikuwa “shaolin temple” 1982.
Alitengeneza filamu nyingine “Born to defend” ambayo ilionesha uhalisia wa maisha ya binadamu ya kawaida lakini haikufanya vizuri sokoni. Li akatoa Shaolin Temple ya pili kabla hajafanya nyingine the folk hero, wong Fei – Hung  akiwa muongozaji , “Once upon a time in china” mwaka 1991. Mwaka 1992 na nyingine mbili 1993 ikiwemo “the Legend of Fong sai – Yuk” na moja 1997.
Jet li alitengeneza filamu inayoendana na filamu aliyotengeneza Bruce Lee ya “Fist of Fury” na yeye kuiita filamu yake “fist of legend” mwaka 1994. Wamarekani walianza kumfahamu alipotoa filamu iliyomtambulisha kwao ya “Lethal Weapon 4” mwaka 1998
Toka kipindi hicho alianza kuingia mikataba na Hollywood na kutoa filamu kama “Romeo must Die (2000)” “kiss of the Dragon” (2001), “Hero” (2002) “war” (2007) na Forbidden Kingdom” mwaka 2008 akiwa na Jackie Chan. Li pia alicheza “Mummy” Jomb of the Dragon Emperor mwaka huohuo
Mwaka 2010 alicheza filamu nyingine kama “ying yang” “Expendables” ambayo ilienda na kutoa Expendables 2 mwaka 2012 akiwa na wasanii wakongwe katika tasnia ya filamu Marekani Sylvester (Rambo), Bruce Wills, Arnold, Van Damme, Dolph na wengine wengi.Alioa mara mbili, mwaka 1987  alioa Huang Qiuyan na kubahatika kupata watoto wawili wa kike Si na Taimi kabla ya kuachana mwaka 1990. Mwaka 1999 alioa mke mwingine ambaye ni mwigizaji maarufu sana Nina Li Chi, waliyezaa naye pia watoto wawili Jane (2000) na Jada (2002)
Jet li alipata maafa Desember 2004, alipokuwa anamwokoa mwanae Jane katika moja ya hotel zake anazomiliki ilipotokea kimbunga cha tsunami na kubomoa jingo hilo. Ilisadikika amefariki dunia lakini yupo hai na alipona yeye na mtoto wake inga yeye aliteguka mguu na kupata majeraha madogo madogo.


No comments: