Alijiunga na chuo kikuu cha Columbia, alikutana na ubaguzi wa rangi umetapakaa New York. Alikuwa kiongozi wa jumuiya wa kanisa moja Chikago kwa miaka 3, akisaidia watu masikini wasio na makazi maalum. Baadae alijiunga na chuo kikuu Havard kusomea sharia, mwaka 1990 alikuwa mwafrika wa kwanza mhariri wa mapitio ya sharia. Pia alianza kufundisha chuo kikuu Chicago kitivo cha sharia na baadae kuoa Michelle Robinson aliyekuwa mfanyakazi mwenzie.
Mwaka 2004 Obama alichaguliwa kuwa Seneta akiwakilisha IIlinois, wananchi walipata hamasa ya kendelea kumfahamu Barrack alipohutubia mkutano wa chama cha demokrasia, Boston. Mwaka 2008 aligombea urais, pamoja na kwamba alikuwa kwenye siasa kwa miaka 4 alishinda kiti cha urais. Mwaka 2009 january aliapishwa kuwa rais wa 44 wa Marekani na kuwa mwafrika wa kwanza kuingoza Marekani.
Alishauliwa na mkewe kuacha kuvuta sigara kutokana na kampeni alizofanya za kugombea urais na yeye kutii na kuacha kabisa.