Oct 26, 2012

MJUE STAA WETU WA LEO!

Obama,_BarackBarrack Hussein Obama II alizaliwa tarehe 4 August 1961 mama mwenye asili ya kizungu nchini Marekani, Ann Dunham na baba wa kiafrika mwenye asili ya Kenya, Barrack Obama Sr. Ann na Barrack walipata motto wao wakiwa bado ni wanafunzi wa chuo kikuu cha Hawaii. Barrack Hussein aliondoka nchini Marekani na kurudi Kenya akawa mchumi wa serikali, huku nyuma akimwacha mwanae na mama yake. Ann aliolewa na mwanaume mwingine raia wa Indonesia aliyekuwa manager wa kampuni ya mafuta (oil), Jakarta Barrack akiwa na umri wa miaka sita. Barrack aliona maisha ya Indonesia ni magumu hivyo alilazimika kurudi nchini Marekani kuishi na babu yake aliyekuwa anafanya biashara ya samani za ndani wakati bibi yake alifanya kazi benki. Familia iliishi katika nyumba za kupanga, pamoja na kipato kidogo walichokipata waliweza kumpeleka shule iliyokuwa juu katika mji wa Hawaii. Alionana na baba yake akiwa ametimiza miaka kumi.

Alijiunga na chuo kikuu cha Columbia, alikutana na ubaguzi wa rangi umetapakaa New York. Alikuwa kiongozi wa jumuiya wa kanisa moja Chikago kwa miaka 3, akisaidia watu masikini wasio na makazi maalum. Baadae alijiunga na chuo kikuu Havard kusomea sharia, mwaka 1990 alikuwa mwafrika wa kwanza mhariri wa mapitio ya sharia. Pia alianza kufundisha chuo kikuu Chicago kitivo cha sharia na baadae kuoa Michelle Robinson aliyekuwa mfanyakazi mwenzie.

Mwaka 2004 Obama alichaguliwa kuwa Seneta akiwakilisha IIlinois, wananchi walipata hamasa ya kendelea kumfahamu Barrack alipohutubia mkutano wa chama cha demokrasia, Boston. Mwaka 2008 aligombea urais, pamoja na kwamba alikuwa kwenye siasa kwa miaka 4 alishinda kiti cha urais. Mwaka 2009 january aliapishwa kuwa rais wa 44 wa Marekani na kuwa mwafrika wa kwanza kuingoza Marekani.

Alishauliwa na mkewe kuacha kuvuta sigara kutokana na kampeni alizofanya za kugombea urais na yeye kutii na kuacha kabisa.




WATANO WATIWA MBARONI KWA MAUAJI YA RPC WA MWANZA...MMOJA AKIRI KUMPIGA RISASI




Mkurugenzi wa makosa ya jinai nchini (DCI) Robert Manumba (mwenye miwani), akitoa taarifa hiyo

Jeshi la polisi Tanzania limekamata watu watano jijini Dar es Salaam kwa tuhuma za mauaji ya aliyekuwa kamanda wa polisi mkoa wa Mwanza Alberatus Barlow na bado linaendelea kuwatafuta watuhumiwa wengine.

Akiongea na waandishi wa habari jijini Mwanza Mkurugenzi wa makosa ya jinai nchini (DCI) Robert Manumba amewataja watu hao kuwa ni muganizi Michael (36) Mkazi wa Isamilo ambae alikiri kumuua kamanda kwa risasi.

Wengine ni Chacha Waitara Mwita (50), Magige Mwita Marwa, Bugazi Edward Kusota na Bhoke Mara Mwita(42). Watuhumiwa hawa walikamatwa baada ya kuwekewa mtego na kwa ushirikiano kati ya jeshi la polisi na wananchi.

Manumba alisema kikosi kazi cha upelelezi kilichokuwa chini yake kilijigawa kwenye makundi matatu, yaani kundi la ukamataji, mahojiano na kundi jingine la intelejensia ambapo walitumia njia ya kisayansi kwa kufuatia mitandao ya simu. Na kwamba jeshi hilo limefanikiwa kukamata bunduki iliyotumiwa kutekeleza mauaji hayo na simu aliyoporwa mwanamke aliyekuwa amesindikizwa na Kamanda Barlow na bado polisi inasaka radio call aliyokuwa nayo marehemu.

Watuhumiwa hao watano wanafikisha idadi ya watuhumiwa kumi wanaoshikiliwa na jeshi la polisi kwa tuhuma za mauaji hayo.

Marehemu kamanda Barlow aliuawa usiku wa Oktoba 12 kati ya saa saba na saa nane eneo la, Kitangiri, Kona ya Bwiru mkoani Mwanza baada ya kupigwa risasi na watu wanaodhaniwa kuwa ni majambazi alipokuwa anamsindikiza mwalimu Dorothy Moses nyumbani kwake.