Aug 12, 2012

MJUE STAA WETU WA LEO!!!

ROBIN VAN PERSIE

Jina kamili anaitwa Robin Van Persie wengi hupenda kumwita RVP, alizaliwa tarehe 6 august 1983, Uholanzi, ana urefu wa futi 6 na inchi 2. Mama yake anaitwa Jose Ras ambaye ni mchoraji na baba yake ni mchonga vinyago. alizaliwa katika nyumba ya wasanii lakini yeye hakutaka kuwa kama wazazi wake hivyo kipaji chake kilijidhihirisha wazi katika mpira wa miguu. ana dada zake wawili Lilly na Kiki jumla kwao wako watatu akiwa ni mtoto pekee wa kiume. 
      Akiwa na umri wa miaka kumi na saba alijiunga na timu ya vijana SBV Excelsior's youth squad mwaka 2001, lakini haikumchukua muda mrefu aliondoka katika timu hiyo mara baada ya kukosekana maelewano na kocha wake hivyo kujiunga na Feyenoord kwa mkataba wa miaka miwili na nusu. Akiwa na timu hiyo alipata tuzo ya KNVB ya kijana mdogo mwenye kipaji mwishoni mwa mwaka 2001/02. Lakini pia hapakuwa na melewano mazuri na kocha wake Bert Van Marwijk hivyo kufanya Van kukaa benchi muda mrefu
     alisaini mkataba mwingine wa mwaka mmoja na Feyenoord 2003/04, hata hivyo bado aliendelea kukaa benchi muda mrefu, ingawa katika mechi alizocheza alifanikiwa kufunga magoli 28 tu yakiwa ni magoli machache sana ukilinganisha na magoli aliyofunga misimu iliyopita. katika usajili mdogo wa january Van Persie aliuzwa na klabu yake baada ya Arsenal kufika dau la paundi millioni 2.75
      Tarehe 17 May 2004 Van Persie alisaini mkataba wa miaka minne na Arsenal. Kocha mkuu  Arsene Wenger alipanga kumbadilisha Van Persie toka winga ya kushoto na kumweka kuwa mshambuliaji wa kati kama alivyofanya kwa Thierry Henry mchezaji wa zamani wa Arsenal, alifanikiwa

      Alikaa sana benchi kwa kipindi cha 2004/2005, alifanikiwa kupata magoli 8 ndani ya mwezi mmoja mwaka 2005 na kutunukiwa zawadi ya kuongezewa mkataba mwingine hadi 2011 January 4, lakini siku mbili baadae alivunjika kidole alipokuwa anacheza fainali za kombe la FA dhidi ya Cardiff.

       Katika medani za kimataifa alifanikiwa kuiongoza vizuri timu yake ya Taifa ya Uholanzi mwaka 2006 katika fainali za kombe la Dunia. aliipa ushindi wa kuingia kumi na sita bora kwa goli lake la pekee alilofunga dhidi ya Ivory Cost. hata ivyo timu iliishia katika raundi hiyohiyo!!
      
       Tarehe 13 June 2005 akiwa na timu yake  ya taifa, Van Persie  alikamatwa kwa tuhuma za ubakaji na muhusika mkuu alikuwa Sandra Krijgsman aliyekuwa Miss Nigeria Holland, hivyo alikaa rumande kwa wiki 2 kisha kumwachia kutokana na ushahidi kutokukamilika lakini uchunguzi ulikuwa unaendelea

      February 2006 kesi iliisha na kufutwa na mahakama ya Jamhuri ya Uholanzi baada ya uchunguzi kukamilika na kukuta hakuna hatia juu ya tuhuma zilizokuwa zinamkabili mchezaji huyu.

     2012 imeingia katika historia mpya kwa Arsenal kumkosa tena mshambuliaji tegemezi aliyeihama timu hiyo na kwenda Manchester  United kwa ada ya paundi millioni 24. hapa tena hakuna mjadala.........!!!
  Swali ni je kuuzwa kwa Robin Van Persie ni  maana ya kwamba timu ya Arsenal haiwezi tena kushindana na klabu kumbwa duniani???

HII INAWAHUSU MASHABIKI WA ARSENAL !!!!   
      

No comments: